MWONGOZO WA KIGOGO Notes
MTIRIRIKO;
ONYESHO LA KWANZA.
TENDO LA KWANZA.
Ni katika karakana ya soko la Chapakazi,Sudi, Boza na Kombe wanafanya kazi ya uchongaji.Sudi amefungulia radio huku wakiendelea na kazi yao.Ashua anawaletea chai ya mkandaa na mahamri na kuondoka.
Habari inatolewa kwa wananchi wa Sagamoyo kuwa wana kipindi cha mwezi mzima kusheherekea uhuru wao, wawaku buke majagina wao waliopigania uhuru na kuwanasua kutoka utumwani, wimbo wa kizalendo unachezwa mara kwa mara.
Sudi anatofautiana na mpango wa kusheherekea uhuru kwa mwezi mzima;kwake majagina wanaosheherekewa hawakufanya lolote katika historia ya Sagamoyo.
Kuna uchafuzi wa mazingira, viongozi hawajawajibika kusafisha soko wanadai kodi na kitu juu pia vitisho kwa wanasagamoyo.
WAZO KUU.
Kuna wale ambao wanaunga viongozi mkono kwa sababu wanafumbwa kwa mambo yasiyo ya kimsingi.Aidha kuna wale ambao wamezinduka na kuhisi kuwa viongozi hawajawajibika. Sudi haoni umuhimu wa sherehe za uhuru kupewa maandalizi ya kifahali na kipindi cha mwezi mzima.
TENDO LA PILI.
Katika karakana sokoni,Kenga anawatembelea Sudi, Boza na Kombe.Ametumwa na Majoka kuchukua vinyago vya mashujaa.Ni msimu wa mashujaa Sagamoyo, Sudi anachonga kinyago cha shujaa wa kike ambaye kwake ni kiongozi halisi wa Sagamoyo.Shujaa huyo hakufanya lolote, bali analifanyak sasa katika jimbo la Sagamoyo.
Miradhi ya kuchonga vinyago inafadhiliwa kutoka nje na wananchi wanatakiwa kulipa baada ya mwaka mmoja.
Sudi anashawishiwa kuchonga kinyago cha Ngao ili maisha yake yabadilike na jina lake kushamiri;aidha apewe likizo ya mwezi mmoja ughaibuni.Sudi anakataa kuchonga kinyago,Kenga anawapa keki lakini Sudi hali kwa kuwa ni makombo.Kombe anazinduka kutokana na kauli hii, anamuunga mkono Sudi.Kenga anaondoka kisha Tunu anawasili huku akihema na kusema kuwa mzee Kenga anapanga njama ya kuhutubia wahuni.Wote wanaondoka.
NAFASI YA MWANAMKE
1. Mwanamke ni katili-
Mamapima anawauzia wanasagamoyo wenzake pombe haramu inayowaua na kuwapofusha Wengine.
2. Mwanamke ni mwenye mapinduzi
Tunu anaongoza harakati za mapinduzi dhidi ya Uongozi dhalimu wa Majoka kwa ushirikiano wa Sudi.
3. Mwanamke ni msomi
Tunu Ana shahada na uanasheria inayomwezesha kutetea haki za Wanasagamoyo dhidi ya Uongozi dhalimu wa Majoka.
Ashua pia Ana shahada ya ualimu lakini anauza maembe sokoni Licha ya kupewa kazi kwenye shule za Majoka and Majoka Academy anazodai Ni za kihuni.
4. Mwanamke ni Jasiri
Licha ya kuvunjwa mguu, Tunu anaendeleza mapinduzi Hadi anafanikiwa kumwondoa Majoka mamlakani.
Pia anafahamu ukatili wa Majoka lakini anamweleza waziwazi kuwa watalipa kila tone la damu walilomwaga Sagamoyo.
5. Mwanamke ni mwenye wivu
Husda anapigana na Ashua ofisini mwa Majoka akidai kuwa amekuja kumnyanganya mume.
6. Mwanamke ni Mwasherati
Mamapima anamgawia ngurumo uroda ili amsaidie kupata kandarasi ya kuoka keki ya Uhuru
7. Mwanamke ni Mwenye uchu
Husda anapomwona Chopi, anaanza kutembea kwa maringo huku akionyesha macho ya uchu.
SWALI LA LEO
Kisimani mmeingia paka, maji hayanyweki tena...
a. Weka dondoo hili katika muktadha wake. (alama 4)
b. Bainisha tamathali ya usemi iliyotumiwa katika dondoo hili. (alama 2)
c. Ukirejelea tamthilia nzima ya kigogo, thabiti kwa mifano kumi na minne ukweli kuhusu wa kauli hii. (alama 14)